.

.

Mjue Mwenza kweli



Mjue Mwenza wa kweli.

 


 Moyo wa mtu ni kama kichaka huwezi kugundua yalimo ndani yake na siku zote jambo usilo lijua ni sawa na usiku wa giza na watu wengi tanadanganyika tukifikiri kuwa kila king’aacho ni dhahabu.

 

Bila shaka u mzima wa afya mpenzi msomaji wa safu hii,usichoke kumshukuru Mungu ukijaaliwa kuiona siku mpya kwa sababu wapo wengi wanaotamani kuiona siku mpya lakini hawakuweza kuiona,sio kwamba wao ni wakosefu mbele za Mungu na wewe ni mwema bali ni kwa neema na mapenzi yake yeye aliye muweza wa yote Mshukuru kwa kila jamabo.

 

 leo katika safu hii  nakuletea mada inayoitwa Mjue Mwenza wa Kweli,nimekuletea mada hii kwasababu najua unapata ugumu kiasi gani kumtambua mwenza bora ususani kwa karne hii ambapo utapeli umeshamiri katika uhusiano,sio wanawake sio wanaume wote wemekuwa hawaaminiani katika suala la kukabidhiana zawadi nzuri ya Upendo.

 

Inawezekana upo katika uhusiano na tapeli wa mapenzi bila kujua, au una mpango wa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu bila kujua kama ni Tapeli hiyo ni hatari, unachotakiwa kufanya sasa ni kuanza kumchunguza mpenzi wako mapema usije kujuta badae kwani wahenga walisema majuto ni mjukuu.  

 


Kumbuka, kuwa katika uhusiano na mtu ambaye haeleweki ni sawa na kukaribisha matatizo katika maisha yako, huna sababu ya kuishi kwa wasiwasi ukiwa hujui mpenzi wako anakuchukulia vipi.

Mpendwa msomaji wa safu ya Mwenza Wa Nani zifuatazo ni sifa za Mwenza bora,zisome na uzielewe kwa makini kuepusha migogoro ya kimapenzi hasa unapoanzisha uhusiano na mtu asiye sahihi ‘wrong person’ wenzetu wanasema.

 

1. Atataka kukutambulisha kwa rafiki zake.

Hii ni kati ya alama ya mwenza bora,atakuwa mtu wa kujivunia kuwa na wewe kila sehemu kwa marafiki zake na hatosita kukutambulisha kwa watu wake wa karibu.

 

2. Sio msiri.

Hii ni alama nyingine aliyonayo mwenza bora.Siku zote atakushirikisha kwenye mambo yake ata kama ni ya kifamilia au kiofisi hatoweza kukuficha.

 

3.Atakuheshimu.

Mwenza wa kweli atauheshimu na pia ataheshimu mawazo na maamuzi yako,hawezi kufanya kitu ambacho kitakuudhi wala kukushushia heshima yako kwa namna moja au nyingine.

 

4.Atapenda kuzungumzia malengo.

Mwenza wa kweli atazungumzia malengo ya uhusiano wenu,na atapenda kutengeneza mwongozo mapenzi yenu pia atakuuliza malengo  yako na vitu muhimu unavyovitarajia katika uhusiano wenu.

 

 5.Atataka ndugu wafahamiane.

 Mapenzi hayaishii kwa nyie wawili pekee bali hata kwa ndugu zenu. Mnapojuana inakuwa rahisi kusaidiana hata katika mambo mengine ya kawaida.Hivyo mwenza wa kweli atataka ndugu wa pande zote mbili wafahamiane na waungane kupitia uhusiano wenu.

 

itandeea.............

No comments:

Powered by Blogger.